Wednesday, 18 December 2013

TUNAYO MATUMAINI KWA OWINO



Safu ya ulinzi ya timu ya taifa imeshuhudia walinzi mbalimbali ambao wamekuja na kupotea lakini mara nyingi safu hii imelaumiwa zaidi kando na ile ya ushambulizi.Tangu  kustaafu kwa Musa Otieno,wengi walipoteza matumaini ya kupatikana tena kwa mlinzi kama yeye.Baadhi ya walinzi ambao walionekana kuvaa viatu vyake na kutusaidia angalau kutwaa taji ni zablon Amanaka,Shikokoti,George Owino,Pascal ochieng,Edgar Ochieng,Julias Owino miongoni mwa wengine.Hata hivyo,katika misimu yao,walinzi hawa hawakufanikiwa kutwaa taji lolote na timu ya taifa,hasa baada ya kustaafu kwa Musa.

Mara ya mwisho timu ya taifa kutwaa kombe lilikuwa mwaka wa 2002 ambapo tulinyakua kombe la CECAFA chini ya uongozi wa Musa Otieno kwenye ulinzi.Lakini baada ya kutwaa kombe hili tena chini ya uongozi wa David Owino 'Calabar' katika safu ya ulinzi,sina shaka kuwa yeye ndiye mridhi halali wa viatu vya sogora Musa.Katibu Mkuu wa klabu ya Owino,Gor Mahia,George Bwana aliwahi kunukuliwa akisema kuwa mchezaji huyu atasalia katika historia ya nchi hii kwani mchezo wake ni wa hali ya juu.

Owino alianza mchezo huu katika akademia ya nakuru All Stars mwaka wa 2004-2008,iliyokuwa ikifahamika kama St. Joseph.Alijiunga na klabu ya Karuturi mwaka wa 2008 hadi 2011 aliposajiliwa na miamba wa soka nchini Gor Mahia.Mchezo wake ulivutia timu ya taifa na kuitwa kwenye vikosi mbalimbali.Mojawapo ya michuano ambayo alifana zaidi ni kati ya Nijeria ambapo alimkaba mshambulizi Mosses na kumnyima nafasi ya kutuadhibu nyumbani kwao.Baada ya mchuano huo,mlinzi wa taifa Arnold Origi alimmiminia sifa tele mchezaji huyu kwenye kurasa ya kitandazi 'Kenya imebarikiwa kuwa na walinzi bora enzi hii,David Owino na David 'cheche' Ochieng'

Ubabe wa mchezaji huyu haikukomea hapo kwani aliisaidia Gor kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Tusker kama mlinzi wa kulia.Pia alisimama kidete na kuwadhibiti washambulizi pinzani kwenye dimba la CECAFA akiwemo mfungaji bora kwenye kitupe hicho wa Sudan,Salah ambayo Kenya ilishinda.Hivi majuzi ametajwa kama mchezaji bora wa goal.com na hivyo kuashiria uwezo wake wa kuisaidia timu hii katika awamu zingine.Mlinzi huyu amepata sifa si haba kutoka kwa wakufunzi mbalimbali,wachezaji na hata baadhi ya wadadisi wa soka nchini.Ama kwa kweli,tukiwa na Owino,ni nini kitatuzuia kushiriki dimba la kombe la bara Afrika na hata kufanya vyema katika shindano hilo?

 

Monday, 9 December 2013

NAMNA TIMU ZA AFRIKA ZIMEDHALILISHWA KWENYE MAKUNDI



Hatimaye uorodheshaji wa timu katika makundi mbalimbali ya Kombe la Dunia utakaoanza mwaka ujao Juni ilikamilika ijumaa iliyopita.Timu zote thelathini na mbili ziligawanywa katika makundi manane ambapo kila kundi ilipewa timu nne.Kama kawaida kuna wale wanafurahia mchakato huo ila hakutawahi kosekana wanaohuzunika pia kwani matarajio yetu huwa tofauti huku kila mmoja akilenga timu wanazozidi ili kuwashinda na kuendelea katika awamu zifuatazo.

Katika shughuli hiyo,timu za Afrika zimepewa mapinzani dhabiti,swala ambalo linatupa wasiwasi ni iwapo kuna timu yoyote kutoka bara hili itafaulu kuvuka awamu ya makundi.Acha tutizame nafasi ambazo timu zetu zinazo katika makundi yao.

      1.KAMERUNI
Iwapo kuna timu ya Afrika ambayo imenyimwa nafasi kabisa basi ni taifa la Kameruni.Kama shabiki sugu wa timu hii,itanibidi nivumilie niombe angalau tusiondolewe bila pointi katika kundi hili la A.Kucheza dhidi ya waandalizi Brazil,Korasia na Meksiko si suala la kutilia hamnazo.
Mibabe hawa wa soka barani watalazimika kutia bidii na kuomba miujiza itendeke katika michezo yao maanake hakuna asiyefahamu ukali wa Brazil hasa kama waandalizi wa kombe hili na iliyosheheni magwiji kama Neymar,Luiz,Ramirez,Dani Alves,Paulinho,Silva n.k.Meksiko pia inawachezaji wa ngazi ya juu wakiwemo Chicharito na Dos Santos,bila kusahau Korasia inayojivunia Modric,Olic na Mandzukic.Eto'o,Song,makoun na Mbia watahitaji kujituma zaidi maanake nafasi ya tatu ndiyo bora zaidi wanayoweza kupata katika kundi hili.

    2. COTE D' IVOIRE
Kando na wenzao Kameruni,timu ya Ivory Coast pia ina mlima wa kukwea katika kundi  la C itakapochuana na kolombia,Ugiriki na Japani.Timu hizi ni za haiba kubwa ulimwenguni na zinajivunia magwiji katika mchezo huu.
Kolombia itawategemea Falcao na Rodrigez kujinasua ilahali Ugiriki itamwangazia mlinzi Samaras na Gekas kufuzu awamu ijayo.Timu ya Japani pia ina wachezaji kama Kagawa,Honda na Okazaki ambao watajituma kufuza kutoka kundi hili.Ni wakati Drogba,Yaya Toure na Kolo Toure kujikakamua zaidi ili wainasue bara hili.Nafasi bora ninayowapa majabali hawa wa Afrika ni ya tatu.

   3. NAIJERIA
Tofauti na wenzao,timu ya Naijeria haijabanwa sana katika makundi kwani mapinzani wao si wenye haiba kubwa kando na Ajentina. Kundi hili la F linasheheni Naijeria,Ajentina,Uajemi na Bosnia.Ama kwa kweli,uongozi wa kundi hili lina mwenyewe,Messi na wenzake,lakini nafasi ya pili bado ni wazi kwa timu tatu zilizosalia.Naijeria ndiyo timu pekee ya Afrika ambayo inaweza kutuwakilisha angalau katika awamu ya kumi na sita bora ila sitarajii wao kuzidi hatua hiyo.Mikel,Matin na wenzao watumie nafuu waliopewa katika kundi hili angalau kufuzu hatua nyingine.Uajemi na Bosnia hawajaonyesha ukali wowote katika soka ulimwenguni na iwapo kutakuwa vihi hivi,basi Naijeria itaungana na Messi na wenzake kutoka kundi hili.

  4. GANA
Timu ya msimu huu wamejipata katika mikono hatari baada ya kuorodheshwa na Ujerumani,Ureno na Marekani katika kundi la G.Kuna wengi tayari wamefutilia mbali uwezekano wa timu hii kufuzu kutoka kundi hili ila kunao wachache wenye matumaini ya kufana kwa Gana.Jambo lililowazi ni kuwa mapinzani wake si wa kumalizia vinyang'anyiro hivi kwenye makundi ila katika hatua za mbele.
Nuer,Muller,Schwistiger,Lahm na Gomez wataiongoza Ujerumani kama kawaida huku Ronaldo na Nani wakiwakilisha Ureno.Dempsy na Bradely wataiongoza nchi ya Marekani huku Gyan na Essien wakijitahidi kuiokoa timu yao kutoka kwa janga hili.Vile vile,timu ya Gana ninaipa nafasi ya tatu kama yao bora zaidi.


 5. ALJERIA
Kama ilvyo na wenzao,timu hii kutoka kusini mwa Afrika watapata wakati mgumu kujinasua kutoka kundi hili la mwisho H pale watakapochuana na Ubelgiji,Urusi na Korea Kusini.Timu ya Ubelgiji imepata umaarufu siku chache zilizopita kwa kuwa na wachezaji hodari kama Fellaini,Vamalean,kompany,Hazard,De Bruyne na courtois.Urusi inajivunia Shirokov na mlinzi Akinfeev pamoja na kocha wao Capello.Korea Kusini inao Jacheol na Lee Keunho.Watakaotegemewa na Aljeria ni pamoja na mlinzi shupavu Mandjid,Sofiane na Medhi.
Mtazamo wangu ni ule ule,nafasu bora ya timu hii kunyakua kutoka kundi hili litakuwa ya tatu ila itabidi wajitume zaidi ili kufikia hapo.


Uchambuzi huu unaashiria kuwa kati ya timu tano za Afrika,timu yenye nafasi bora ya kufuzu na kutuwakilisha katika awamu ya kumi na sita bora ni Naijeria.Wimbo utakuwa ni ule ule,tushabike timu zetu ila kombe tuwaachie wenyeji.Kila la heri timu za Afrika katika maandalizi yenyu.






























Monday, 2 December 2013

KELI ANATOSHA


Keli akimbia na mpira katika mojawap
 ya michuano ligini

Wapenzi wote wa soka nchini hasa wanaoshabikia timu ya taifa Harambee Stars watakubaliana nami kuwa timu yetu imekuwa ikimkosa mshambulizi wa kuziba pengo lililoachwa na Denis Oliech ambaye mchezo wake umedorora kwa michuano kadhaa iliyopita.Aidha,si kwamba hakukuwa na mshambulizi yeyote katika miaka iliyopita ila tu kati ya waliokuwemo,hamna aliyeonyesha ukakamavu katika safu hiyo.Oliech ni mshambulizi bora nchini na si kwa sababu yake kucheza ulaya ila mabao na michango ambayo ameipa timu ya taifa ndiyo inampa uzito huo na hii ndiyo maana anazidi kuitwa kwenye kikosi cha Harambee Stars hata ingawa umri wake umekolea.
                        

                                                     
JAWABU
Hata hivyo utaafikiana nami kuwa uhaba huu tayari unafika ukingoni kila tukimsikia Jacob Keli.Juzi nikitizama mchuano kati ya timu yetu na Sudan Kusini,shabiki mmoja alizungumza kwa sauti na kusema kuwa Oliech hatapata nafasi kwenye kikosi cha timu hiyo tena.Shabiki huyu hakuwa mbaguzi ila mchezo wake Keli ndio ulimchochea kusema hayo.Ni washambulizi wangapi wameonekana kutwaa nafasi hiyo ila kutupotezea matumaini?Si John Baraza,Mike baraza,Francis Ouma,Kemboi,Obadiah Ndege,Geoge'Black Berry',Lavatsa,Wanga,Were n.k.Orodha hii ni ndefu ila hakuna kaiti yao aliyetupa kiburi cha safu ya ushambulizi kama Oliech.Japo Were bado hajachezeshwa katika timu ya taifa,lakini hivi sasa,mkombozi wetu ni Jacob Keli.

                                                             Kazi zake

Keli apokea tuzo la mfungaji bora ligini
Hatumzungumzii Keli kwa sababu waliojaribu hapo awali walishindwa ila ni kwa ajili ya kazi aliyoifanya.Msimu uliopita,Keli alikuwa mfungaji bora wa ligi ya taifa kwa mabao kumi na saba,mabao mawili mbele ya mwenzake wa Tusker Jese Were.Isitoshe, Keli alitawazwa mshambulizi bora ligini na hatasahaulika kwa kuwanyanyasa mabeki wa Gor Mahia kwenye mchuano wao wa mwisho ligini ambapo alifunga bao moja na kukosa nafasi nyingi ingawa walishinda kwa mabao mawili bila jawabu.Hivi maajuzi,Keli pia alijitoa mhanga kusaidi nchi hii kuilaza Sudan Kusini.Katika mchuano huo,Keli alifunga bao moja na kuwasumbua mabeki wa mapinzani kila mara akiwa na mpira.

Dimba la CECAFA bado linaendlea na iwapo tutautwaa ubingwa huo,basi itakuwa ni usaidizi wa Keli.Mkufunzi wa taifa adel Amrouche anafaa kumtumia mshambulizi huyu hasa kwa kumwanzisha maanake mechi yetu na Ethiopia ambayo tulitoka sare ya kutofungana,Keli alichezeshwa kipindi cha pili ingawa haikumtosha kujituliza na kuonyesha makali yake.Ninatumai kocha huyo atamtumia vilivyo maanake kufikia sasa,KELI ANATOSHA.